Advertssssss

Advertssssss

Menu drop

Monday, December 16, 2013

SEKTA YA MADINI NA UGATUAJI



Na, Doris meghji  Jumanne Disemba 17,2013
Singida – Sekta ya Madini
Bendera za halmashauri ya wilaya ya Singida (picha na Doris Meghji)


Halmashauri ya wilaya ya Singida zinatarajiwa kunufaika kutokana na mpango sera ya ugatuaji (Decentralization by Devolution) wa sekta ya madini nchini kwa serikali kuzitaka halmashauri kuzingiza shughuli za uchimabaji wa madini kwenye mipango yako kwa maendeleo ya wilaya hizo
 
MMWENYEKITI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SINGIDA MH. DIWANI MNYAMPANDA KATIKA WARSHA YA WADAU SEKTA YA MADINI (Picha na Doris Meghji)
Kunufaika kwa halmashauri ya wilaya ya Singida kunakuja kutokana mpango wa kuingiza shughuli za madini katika mfumo wa mpango wa maendeleo ya halmashuri, hivyo kuipa fursa sekta ya madini kushiriki kikamilifu kutoa mchango wake katika maendeleo ya halmashauri
Dr. Mataro Sabai Mshauri mkuu EBF mwezeshaji wa warsha ya wadau wa sekta ya madini halmashuri ya wilaya singida Picha na Doris Meghji)


Kijiji cha Mpambaa ndani ya halmashauri ya wilaya ya Singida kutainufaisha halmashauri hiyo kwa uwepo wa wachimbaji wadogo wa madini katika eneo hilo kupitia sera ya ugatuaji katika sekta ya madini nchini
wadau wa sekta ya madini  halmashauri ya wilaya ya Singida katika warsha ya ugatuaji wakitoa maoni katika vikundi (picha na Doris Meghji)


haya yamejitokeza katika warsha ya wadau wa sekta ya madini wilayani singida yaliyofanyika katika ukumbi wa mikutano wa halmashuri ya wilaya ya Singida chini ya uwezeshaji wa Dr Mataro Sabai mshauri mkuu toka kampuni ya Economic and Business Foundation (T) LTD ya jijini Dar- es- salaam ikiwa ni mpango wa maendeleo ya sekta ya madini katika kipindi cha  2014/15  hadi 2015/16.
mmoja ya kundi la wadau wa sekta ya madini katika warsha ya wadau wa madini halmashuri ya wilaya ya singida wakijadili mambo ya kuandaa mipango na muongozo


Kwa mujbu wa sera hiyo ya ugatuaji lengo la serikali kupeleka sera hiyo ya sekta ya madini ni kuhakikisha shughuli za uchimbaji zinaingizwa kwenye mipango ya halmashauri ili iweze kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya wilaya 
kundi lingine la wadau wakijadili mambo muhimu ya kuweka katika mipamgo na muogozo wa ugatuaji (picha na Doris Meghji)


Aidha ushirikishwaji wa sekta ya madini katika maendeleo ya wilaya kutaharakisha maendeleo ikiwa ni pamoja na kutoa huduma hususini zinazotakiwa kwa maendeleo ya wachimbaji wadogo
mmoja wa washiriki katika kundi bajeti akiwasilisha bajeti ya kuendesha sekta ya madini katika mipango ya maendeleo ya halmashauri (Picha na Doris Meghji)
 

Kwa upande wa washiriki na wadau wa warsha hiyo maoni mbali mbali ya ugatuaji ya sera katika sekta ya madini yametoliwa ni pamoja na malengo ya kuwepo kusajili na kuwatambua wachimbaji wadogo,kuwa sheria ndogo za kijiji zinazowezesha kijiji na halmashauri husika kunufaika na shughuli za uchimbaji madini na kuimarisha huduma za jamii katika maeneo ya wachimbaji madini na inayozunguka migodi.
washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia uwasilishwaji wa mipango mbali mbali katika ugatuaji wa sekta hiyo kwa halmashuri(Picha na Doris Meghj)

Kwa upande wa mikakati wadau wa sekta ya madini katika warsha hiyo amependekeza upatikanaji wa huduma za mawasilino za uhakika katika maeneo ya madini,bara bara za uhakika zinazopitika majira yote ya mwaka kwenda kwenye maeneo ya wachimbaji wadogo wa mpambaa na maeneo ya masoko ya madini ikiwa ni pamoja na kuimarisha huduma za afya maeneo ya wachimbaji 



Aidha suala la mafunzo kwa wachimbaji wadogo 70 halikusaulika katika warsha hiyo kwa wachimbaji wadogo kupatiwa mafunzo juu ya jinsi ya kuendesha shughuli za madini kwa tija na namna ya kupata mitaji kutoka kwenye vyombo vya fedha
wadau wakifuatila mambo ya kuweka katika mipango na muongozo wa ugatuaji wa sekta ya madini katika halmashauri ya wilaya ya singida (picha na Doris Meghji)



Hata hivyo kwa wakati huu shughuli za madini kwa kiasi kikubwa zinafanyika nje ya mfumo wa mipango halmashuri, na  maeneo ya madini kutohudumiwa ipasanyvo kwa kuwa shughuli hizo kisheria ziko nje ya uwezo wa halmashuri. Hivyo ugatuaji huo utasidia kusogeza huduma karibu na jamii kwa halmashauri husika kutoa huduma hizo kwa wadau wa sekta hiyo.
mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya singida Mh.  Nyampanda Diwani wa kata ya Mtinko akifunga warsha ya wadau sekta ya madini (picha na Doris Meghji)

Madini ya dhahabu,shaba,fedha,mchanga mawe na kokoto yamegundilika katika halmashauri hiyo hasa katika eneo la Mpambaa 
Mwisho.

Sunday, December 15, 2013

Safari ya mwiso ya Nelson Rolihlahla Mandela

Oprah Winfrey pamoja na waombolezaji wengine wakifuatilia maziko ya Rais mzalendo wa kwanza wa Afrika kusini Nelson Mandela kijiji Qunu katika jimbo la Eastern Cape

Jeneza lililobeba mwili wa Raisi wa kwanza wa Afrika kusini likiwa linawasili eneo la maziko katika kijiji cha Qunu

Jeneza likiwa limepambwa kwa bendera ya Afrika kusini pia chini pakiwa pametandikwa ngozi ya ng'ombe
Hapa ndipo ilifanyika sala kabla ya kuelekea makaburini

Mizinga ishirini na moja ilipigwa kuonesha heshima kwa Rais wa kwanza mzalendo Nelson Rolihlahla Mandela

Rais mstaafu wa Afrika kusin Thabo Mbeki akisalimia na Askofu mstaa na mshindi na tuzo yz amani ya Nobel Desmond Tutu

Muombolezaji akifuatilia maziko kijijini Qunu

Mjane wa Nelson Rolihlahla Mandela,Graca Machael akiwa na majonzi wakati wa mazishi

Hapakuwa na tofauti, Winnie Madikizela Mandela akimshika Graca Michael kuaga jeneza na Rais mzalendo wa kwanza Nelson Rolihlahla Mandela

Mandle Mandela kiongozi wa kimila wa ukoo wa Mandela

Rais Jacob Zuma akihutubia waombolezaji

Winnie Madikizela Mandela,Rais Jacob Zuma na mjane wa Rais mstaafu wa Afrika kusini Nelson Rolihlahla Mandela Graca Michael wakiwa na nyuso za huzuni
R.I.P TATA NELSON ROLIHLAHLA MANDELA
1918-2013

Friday, December 13, 2013

WANAWAKE NA VIJANA WAPATIWA ELIMU YA UJASILIAMALI- MANISPAA YA SINGIDA

Na, Doris Meghji  Ijumaa  Disemba 13 ,2013

Singida


Wanawake wametakiwa kutumia elimu ya ujasilimali ili kujikwamua kiuchumi kwa kuwa wanawake ndio walezi wakuu wa familia nchini

Afisa Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Singida Bi Hanna Churi amewaasa wanawake hao katika mafunzo ya ujasilimali yaliondaliwa kwa wanawake na wanachama wa jumuhiya ya wanawake wa Chama cha Mapinduzi(UWT) wilaya ya singida mjini kwa uwezeshaji toka shirika la kazi duniani (ILO) kupitia mpango wa kazi nje nje yanayofanika katika ukumbi wa chuo cha maendeleo ya wananchi manispaa ya Singida 

Bi Hanna Churi na mwenyekiti wa muda katika mafuzo ya ujasiliamali yaliofanyika chuo cha maendeleo ya wananchi manispaa ya singida (picha na Doris Meghji)


Aidha Bi Churi amewataka wanawake hao kutumia fursa ya  mafunzo ya ujasiliamali yakayowawezesha kutumia mbinu mbali mbali katika kubuni miradi na kutafuta masoko ikiwa ni pamoja na kuimarisha mahusiano ndani ya jamii 
 
MH. DIWANI WA KATA YA UTEMINI BARTAZAR KIMARIO, KATIKATI MGENI RASMI BI HANNA CHURI AFISA MAENDELEO YA JAMII MANISPAA YA SINGIDA KWENYE MAFUNZO YA UJASILIAMALI - WANACHAMA WA UWT - SINGIDA MJINI ( picha na Doris Meghji)




BAADHI YA WASHIRIKI WA MAFUZNO YA UJASILIAMALI - UKUMBI WA CHUO CHA MAENDELEO YA WANANCHI (FDC) SINGIDA ( picha na Doris Meghji)

Kwa mujibi wa Afisa Maendeleo wa Jamii huyo anasema “ kwa kupitia mafunzo haya ya siku tatu hii itawasidia kujenga na kuimarisha mahusiano kati yenu na kuwa na sauti mmoja ndani ya jamii kwa kukutwanishwa pamoja katika mafunzo haya ya  ujasiliamali alisisitiza Bi Churi
AFISA MTENDAJI KATA YA UTEMINI BI EVA MBELWA NA KIJANA ANTONIA KATIKA MAFUNZO YA UJASILIAMALI - YALIOANDALIWA NA UWT SINGIDA MJINI (picha na Doris Meghji)

Awali akisoma taarifa ya uandaaji wa mafuzo hayo ya ujasiliamali  Katibu wa UWT wilaya ya mjini Bi Margaret K. Malecela ameeleza lengo la kuandaa mafunzo kwa wanawake na wanachama wa jumuiya hiyo ni kuwaendeleza wanawake katika kujikwamua kiuchumi na kujenga taifa lisilotegemezi kupitia elimu hiyo ya ujasiliamali 
KATIBU WA UWT WILAYA YA SINGIDA MJINI BI MARGARET MALECELA AKIWA NA MWENYEKITI WA MUDA NA MGENI RASMI WA KUFUGUA MAFUZO HAYO HANNA CHURI AKIWA PAMOJA NA DIWANI WA KATA YA UTEMINI MH. BARTAZARI KIMARIO (picha Doris Meghji)
Naye diwani wa kata ya Utemini ambapo mafunzo hayo yanafanyika Mh. Bartazari Kimario ameweataka wanawake hao kuyatumia mafunzo hayo vizuri ili yawasaidie katika kuliendeleza taifa hili la Tanzania kwa kuwa wanawake ndio tegemeo la familia na taifa kwa ujumla.
Bi REHEMA SHILLA NA BAADHI YA WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UJASILIAMALI YALIYOANDALIWA UWT -WILAYA YA SINGIDA MJINI ( picha na Doris Meghji)


Katika kuendesha mafunzo hayo ya ujasiliamali Mwezaji Lilian Nkida na Godwin Hillary toka shirika la kazi duniani (ILO) kupitia mpango wa kazi nje nje wamesema mafunzo hayo yatalenga maeneo makuu manne ambayo ni kujitambua, kubadilika kimtazamo,kubuni wazo la biashara na kuanzisha biashara yako.
WASHIRIKI WA MAFUNZO YA UJASILIAMALI - YALIYOANDALIWA NA UWT -SINGIDA MJINI NA KUWEZESHWA NA ILO - KITENGO CHA KAZI NJE NJE.(picha na Doris Meghji)

Hata hivyo kupitia mpango huo wa serikali unaosimamamiwa na shirika la kazi duniani ILO zaidi ya vijana na wazee 800 wamepata mafuzo hayo mkoani Singida
Lilian Nkinda mwezeshaji wa mafunzo ya wanawake wa UWT- Singida mjini Kutoka ILO kitengo cha kazi nje nje(Picha na Doris Meghji)


Zaidi ya washiriki 25 toka wilaya ya singida ya mjini wamehudhuria mafunzo haya ya siku tatu yalionza jana na kumalizika kesho katika ukumbi wa chuo cha maendeleo ya wananchi manispaa ya singida 

KIJANA GODWIN HILLARY MWEZESHAJI WA MAFUZO YA UJASILIAMALI TOKA SHIRIKA LA KAZI DUNIANI  (ILO) KITENGO CHA KAZI NJE NJE(picha na Doris Meghji)

Hata hivyo kupitia mpango huo wa serikali unaosimamamiwa na shirika la kazi duniani ILO zaidi ya vijana 700 wamepata mafuzo hayo mkoani Singida

MWISHO

Wednesday, December 11, 2013

Safari ya mwisho ya Nelson Mandela katika misa maalum

Wakuu wa nchi mbalimbali duniani wawasili Afrika ya kusini kwa ajili ya safari ya mwisho ya Nelson Mandela

Raisi wa Marekani Barack Obama na mkew Michel Obama wakiwasili Afrika kusini kwa ajili ya kuhudhuria safari ya mwisho ya Nelson Mandela

Askofu Desmond Tutu mshind wa tuzoya nobeli ya amani

Katibu mkuu mstafu wa Umoja wa Mataifa Koffi Atta Anan akiwa na Askofu Desmond Tutu wakati wa misa maalum ya kumuombea Nelson Mandela


Baadhi ya wageni waalikwa katika misa ya kumuombea nelson Mandela katika uwanja wa FNB(Soccer city)

Raisi wa Marekani Barack Obama na mkewe wakifuatilia jambo wakati wa misa maalum



Pamoja na hali ya hewa kuwa mbaya watu walifuatilia misa waliwa na miavuli


Winnie Mandela na Graca Michael wakiomboleza msiba








Winnie Madikizela mandela pamoja na familia yake wakiwasili katika uwanja wa FNB kwa ajili ya misa maalum ya kumuaga baba wa taifa la Afrika Kusini Nelson Mandela



Friday, December 6, 2013

Na Evarista Lucas,
Singida
Alhamis Des 06,2013
Wadau wa sekta ya madini katika Halmashauri ya wilaya ya Singida, wameitaka wizara ya madini na nishati Tanzania  kuboresha maeneo muhimu ya huduma kwa wachimbaji wadogo Mkoani hapa.
Wakitoa maoni yao mapema leo katikasiku ya mwisho ya warsha ya Wadau wa madini iliyofanyika katika ukumbi wa mikuta no wa Halmashauri ya Singida; wamesema ili sekta hii iwe na mafanikio ni lazima miundo mbinu yote ikiwemo maji, bara bara, umeme, mipango miji/vijiji na  huduma za afya iboreshwe ili kukidhi mahitaji ya wachimbaji wadogo.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Singida Ndg Mnyampanda na mwezeshaji  Dr Mataro Sabai wakifuatilia jambo.Picha na Doris Meghji
Uanzishwaji wa vituo vya madini darasa ambavyo vitatumika katika kutoa elimu kwa wachimbaji katika hatua zote za uchimbaji, uaandaji na uchenjuaji wa madini ili kurahisisha kazi yao na kuepuka gharama za  kuyasafirisha nje ya mkoa kwa ajili ya kuyatengeneza.
Sanjari na hayo; wadau hao wamependekeza kuwa licha  ya kuboresha maeneo hayo nyeti, kuwepo na uwiano wa kijinsia katika shughuli za uchimbaji wa madini na umiliki wa vitalu vya machimbo.
Akifafanua juu ya hili mmoja wa wadau hao Bwana Elia Digha amesema; uwiano huu utawekwa kwa wizara kuwwawezesha haswa wanake ili nao wapate kushiriki katika uchimbaji wa madini kwa kuwapatia mitaji na mafunzo.
Wadau wakifuatilia wa sekta ya nishati na madini wakifuatilia mjadala.Picha na Doris Meghji
Digha amesema wanawake wengi wamekuwa wakiogopa kufanya kazi za uchimbaji kwa kuwa kazi kama hiyo inahitaji ujasiri.
Aidha; wadau hao wameongeza kusema kuwa ili wachimbaji hao wadogo waweze kufanikiwa watahitaji kupewa taarifa za mara kwa  masoko haswa bei za madini ili kuepusha suala la kuuza madini kwa bei ya chini.
Warsha hiyo ya siku tatu ambayo iliyoshirikisha madiwani, watendaji wa halmashauri na serikali  kuu na wafanyabiashara ; ilifunguliwa Desemba 3mwaka huu hapa mkoani singida  na kumalizika leo; ikiwa na lengo la kuwashirikisha wadau wa sekta ya madini katika kutoa maoni na kuandaa mpango katika kuchangia maendeleo ya wilaya kwa kupitia Sekta ya madini amabapo wilaya zitanufaika na shughuli za uchimbaji wa madini kwa kujiongezea pato.
Washiriki wa mafunzo ya ugatuaji wa madaraka sekta ya Nishati na Madini wakiwa katika mjadala ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Singida.Picha na Doris Meghji
 
Wadau wa Nishati na Madini wakifuatilia mjadala
Mpango huu wa maendeleo ya Sekta ya madini kwa kipindi cha mwaka  2014/2015 – 2015/2016 umekuwa ni muafaka kwa Mkoa wa Singida ambapo ugunduzi wa madini umefanyika  katika maeneo mbali mbali ya Wilaya hususani maeneo ya Mpambaaambapo madini yaliyogunduliwa na pamoja na dhahabu, shaba na fedha, mchanga, kokoto na mawe.
MWISHO